Afrikaans (Suid-Afrika)

منبرٌ كبيرٌ لنشر وسطية الأزهر الشريف بكل لغات العالم

 

تجريبي
Anonym
/ Categories: Main_Category

تجريبي

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu

Namshukuru Mwenyezi Mungu, sala na amani ziwe kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu pamoja na jamaa zake Masahaba wake na wale waliofuata uongofu wake.

Wageni waalikwa!

Assalaam Alaikum Warahmatullah Wabarakaatuh

Amani iwe kwenu na rehema za Mwenyezi Mungu na Baraka zake.

Karibuni sana katika Al- Azhar Al-Sharif, na kwa mwaliko wa Baraza la Wazee wa Kiislamu, karibuni wageni wetu kutoka Baraza la Makanisa Duniani, na ujumbe wake ambao unawakilisha pande zote za Ukristo Ulimwenguni, kwa kuanza na Dk.  Olaf Fix Tavet - Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa Duniani, Baraza la Wazee wa Kiislamu lilimgundua tokea dakika ya mwanzo tulipomwona huko Geneva, …… - tukagundua kwamba yeye ni mwenye moyo uliojaa kheri kwa wote - ni mwenye ukweli kwa watu wote kuishi kwa amani na furaha kwa maana zake zilizo bora zaidi, Inayopelekea raha na utulivu wa nafsi, na huu ndio ujumbe wa Dini za Kiungu, mizizi yake ni ya pamoja ambayo inagawanyika kutokana na mizizi hiyo sheria zote za dini, na vyote vitokanavyo na sheria kama vile imani, ibada, matendeano na maadili..

Waheshimiwa, ninaomba muniruhusu nianze hutuba yangu mbele yenu kwa kukumbusha yale yaliyofikiwa ndani ya kikao chetu cha kwanza mwaka jana kule Geneva mwezi October 2016, nayo ni: kuongeza juhudi kwa ajili ya kupambana na vipingamizi ambavyo vinasimama katika njia ya uenezaji amani, uadilifu na upendo kati ya watu ndani ya Mashariki na Magharibi, kutimia kwa kikao chetu kijacho - nacho ni kikao cha leo - ndani ya Al-Azhar jijini Cairo, kisha kukamilika kwa mawasiliano ya ana kwa ana na kufikia kwa maudhui ya leo ambayo ni: (Duru ya Viongozi wa Dini katika kusimamia mpango wa utaifa na kuishi pamoja).

Katika maudhui hii vile ninavyodhania - huwenda nitakuwa ni mwenye makosa - ni maudhui inayoonekana kuwa ni yenye umuhimu mkubwa kwa viongozi wa kidini katika Mashariki yetu ya Kiarabu na Kiislamu, kwani ni changamoto kubwa ya hivi sasa ni katika wigo wa miito ya kigaidi na mitazamo yake ambayo inajaribu kupotosha akili za vijana Mashariki na Magharibi na kubebesha katika akili za vijana taswira zao zenye makosa kuhusiana na fikra: (Dola ya Kiislamu) na jaribio la kurejesha uelewa na misamiati iliyoachwa na Fiqhi ya Kiislamu na Sheria ya Kiislamu tokea kudondoka utawala wa (Othmani) 1924 nayo ni kama maneno: watu wa dhimma (watu wa ahadi), Jizya,  mateka...nk.

Na ikiwa mfumo wa ukhalifa wa kiislamu ndani ya vipindi vilivyo pita ulikuwa unaendeshwa na baadhi ya sheria maalumu - zilihukumu kwa mantiki ya zama hizo -  kwa yale yanayofungamana na haki za wasiokuwa Waislamu ndani ya dola la mfumo wa ukhalifa, ni katika mantiki, lakini pia ni katika Fiqhi ya Kiislamu kuwa, mfumo huu wa kisiasa pindi unapobadilika basi hubadilika pamoja nao hukumu nyingi - au chache - zinazofungamana na mfumo huu na kusimama kwa misingi yake ya uhusiano kwa asiye kuwa Mwislamu ndani ya dola ya Kiislamu.

Ndani ya changamoto hizi ambazo zinajaribu kurejesha mifumo ya utawala wa kisasa ndani ya madola ya Kiislamu na kwenda kwenye mifumo ya dhana ndani ya akili zao, ambapo hakuna sababu wala nasaba kati ya mifumo hiyo na Sheria pamoja na Fiqhi yake, bali mahusiano yake na Sheria ya Kiislamu yapo mbali pamoja na maandiko matakatifu pia, na kutokana na hilo tumefahamu ukubwa wa hatari ambayo inafungamana na uelewa huu mbovu na kuendesha Dini kwa udanganyifu ambapo inachanganywa kati ya misingi ya dini iliyokingwa na makosa ndani ya Qurani Tukufu na Hadithi Sahihi za Mtume S.A.W., na kati ya juhudi za wanachuoni ambazo zimelazimisha hali ya zama zilizopita, pamoja na tofauti hizi, matatizo na hali pamoja na mahitajio ya mabadiliko inakuwa kadhia ya: (Utaifa) ndiyo kadhia ya kwanza ambayo yapaswa kuzungumzwa na viongozi wa Dini, kwa sababu yenyewe ni jibu juu ya hali hii ya (udanganyifu) ambayo inapata ufadhili wa kifedha uliowapelekea hawa wadanganyifu, kufanya kazi ili kufikia udanganyifu huu kuwa ni jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na kuurejesha Uislamu katika zama za utukufu na nguvu, sina shaka yoyote kwamba Utaifa ndio mdhamini mkubwa wa kutekeleza kanuni ya Kifiqhi kwa wasiokuwa Waislamu, ninamaanisha kanuni: (wana wao yetu sisi na juu yao yaliyopo juu yetu) na kuyafasiri kwa lugha yetu ya kisasa: usawa wa moja kwa moja katika haki na wajibu .. na ninafuraha ya kusema: Al Azhari Al-Sharif na Baraza la Wazee wa Kiislamu walifanya pamoja mkutano ndani ya mwezi wa pili uliopita kuhusu maudhui hii, chini ya anwani: (uhuru na utaifa… aina mbali mbali na ushirikiano) na palitangazwa kwa mara ya kwanza ndani ya kipindi chetu cha hivi sasa: kuwa mfumo wa utaifa ni mfumo halisi wa Kiislamu, aliutekeleza Mtume S.A.W. mwanzoni mwa dola la Kiislamu, nalo ni dola la Madinat Al Munawara.

Lakini - nategemea nisiwe mwenye kukosea pia - mfano wa wito huu huwenda ukakosa kuwaangazia wengi kwa nchi za Magharibi, kwa sababu utaifa kwao huwenda isiwe ni changamoto ndani ya jamii ambayo inasimama kwa mfumo wa utaifa na kuwa sawa haki na wajibu.

Na huwenda ilikuwa changamoto zaidi huko ni (kupambana) na tukio la Islamophobia. Nalo ni tukio lenye hatari sana pindi likiachwa likiteleza mfano wa mpira wa kwenye barafu pasi ya kutolewa maelezo ya ukweli wa dini na falsafa zake na makusudio yake katika kumfurahisha mwanadamu na kumwinua kwenye ukamalifu wa kiroho, kiakili na kimaadili, na ninaogopa zaidi katika vile niviogopavyo ni kuendelea kwa tukio hili la (Islamophobia) leo, na kuwa (diniphobia) kesho, anga imefunikwa na mawingu meusi ambayo yanapingana na dini, na hasa: dini mbili kubwa: Ukristo na Uislamu.

Ukristo - kwa yale wayasemayo walinganiaji wenye msimamo mkali - ndio dini ambayo ilianzisha vita vya msalaba katika eneo la Mashariki, na kuanzisha vita vya kidini huko Magharibi; na dini ya Uislamu ndiyo dini inayoeneza ugaidi na mauaji ya maangamizi, pamoja na kulipua kwa watu wapenda amani, na kubadilisha maisha ya watu kwa kuyatia woga na hali ya wasi wasi, na wala hakuna ufumbuzi - katika yale wanayodhania wapingaji Uislamu  - isipokuwa ni kuziondoa dini mbili moja kwa moja toka katika maisha ya watu, pindipo hawa wanataka usalama ,amani na maisha yenye utulivu .. na hawa hawatuambii sisi: nini matokeo ya vita ambavyo dini haikuwa na mkono wake kwa karibu wala kwa mbali? Ambavyo vita hivyo viliwashwa na wapingaji na wakataaji wa dini, na dini haikuwa na ngamia wala chochote kama usemavyo mfano wa Kiarabu. Hakika mwenye kuendesha mauaji ya madhehebu ya kijamii ya sasa, ndani ya zama zetu hizi, itambainikia nambari za hesabu: Historia haikukusanya idadi kamili ya wahanga wa dini tokea zama za zamani mpaka zama za hivi sasa, ambapo makumi kwa makumi ya wahanga ambao wamepotea, mamilioni walio uwawa, kukimbia na kuadhibiwa katika njia ya utabirikaji wa uwongo na wala haukuthibiti utabirikaji hata mmoja, na lile lililothibiti baada ya thamani hii kubwa ni kuwa, utabirikaji huu umeendelea mpaka - wakati huu kuwa ni wino kwenye karatasi, bali umebakia kuwa hauwezekani kutekelezwa.

Na muniwie radhi ikiwa nimerefusha kidogo katika kujenga taswira ya wasiwasi wangu unaofungamana na mustakabali wa dini, na kufanya kazi ujumbe wake ambao waliaminika watu wake na wanachuoni wake wenye kulingania uongofu, na sisi sote tunafahamu maandalizi yasiyo ya kimaadili ambayo yameandaa kuharibu dini na kumaliza madhumuni yake, ambayo yamejikita pamoja na masikitiko makubwa katika mwenendo wa vijana, na kulindwa na kanuni. Kupewa sababu na jamii na kutangazwa na utandawazi, yote hayo ni maandalizi yatakayo pelekea ima hivi sasa au hapo baadaye mapigano makali kati ya Waumini na wasiokuwa Waumini.    

Matatizo ya dini za mbinguni hivi leo hayawezi kupatiwa ufumbuzi kwa mapigano kati ya wana dini, lakini hatua ya kwanza ya ufumbuzi - kwa mtazamo wangu - ni kuondoa hali ya wasi wasi kati ya wana dini, na urithi wa kihistoria ambao haifai kwenda sambamba na athari zake mbaya, au kuzileta ndani ya wakati ambao tunapambana ndani yake na vita vya muda mrefu na maadui wa dini… na mbele mpiganaji anayejiandaa vizuri ili kumeza wote.

Na kutokana na lengo hili ambalo tunaliweka mbele ya macho yetu, nikimaanisha: kufahamiana kati ya Asasi za dini, Al-Azhar yenyewe imefanya juhudi ya kukutana na viongozi wa taasisi kubwa za dini ndani ya Ulaya, Vatican, Uingereza, Geneva, Florence, Paris na Berlin. Na kutuma misafari ya amani na kuzunguka miji mikuu mingi duniani ndani ya bara la Asia, Ulaya, Afrika na Marekani…

Ndugu Waheshimiwa! Sisi hapa ndani ya Al-Azhar tunafanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya ndugu zetu na wananchi wetu Wakristo wa Misri, na munapaswa kuzingatia vizuri (Nyumba ya Familia ya Misri) ipo hapa ndani ya makao makuu ya Al-Azhar, na munapaswa pia kulisoma tangazo la mwisho la Al-Azhar kuhusu Utaifa na kuishi pamoja, ambalo linaelezea kuhusu Utaifa badala ya msamiati wa wachache ambao Azhar imeshauacha na hakuna haja ya kurejewa tena, ninadhani hizi ni hatua mbili zilizofikiwa, na zitafuatiliwa na hatua zengine zipo njiani Mwenyezi Mungu akipenda…

Ni matarajio yangu kwa ndugu zangu, kutoamini uzushi na uongo wa vyombo vya habari ambavyo vinahusisha ugaidi na Uislamu, na kuwatuhumu Waislamu kuwatesa wananchi wenzao katika ndugu zao Wakristo, na Uislamu – au Al Azhar katika tukio la uigizaji wao wa fedheha - nyuma ya milipuko miwili ya kigaidi ya hivi karibuni, mfano wa uwongo kama huu bado unahadai juu ya akili inasoma matukio na yaliyo nyuma yake usomaji sahihi, wala nisingependa kupoteza wakati wenu wenye thamani kutoa uthibitisho juu ya uwongo ambao umevuka mipaka, lakini nimeangazia kidogo juu ukweli mmoja tu unathibitishwa na uhalisia uthibitisho wa namba za hesabu, na ninamaanisha kuwa, ugaidi unaua Waislamu na Wakristo, na mkitaka ushahidi ambao hauna utata wala mjadala, basi nendeni kwenye vituo vya takwimu na mlinganishe idadi ya wahanga Waislamu na Wakristo nchini Irak, Syria, na hasa Misri, na mtafahamu baada ya hapo kuwa ugaidi hauna dini wala taifa, na wenyewe wala haujali katika kumwaga damu kuwa hii ni damu ya Mwislamu ambayo inamwagika au damu ya Mkristo, kanisa, soko au mkusanyiko mdogo wa watu wasio na hatia.

Hapa! Al Azhar imedhamiria kulitaka Baraza la Makanisa la Kimataifa huko Geneva kuendesha mapambano dhidi ya Islamphobia, iendeleze hatua zake kuelekea kwenye mazungumzo ya Wakristo Waislamu ambayo yameanzishwa na baraza hili kwa mazungumzo rasmi ya kwanza mwaka 1982 kati ya Baraza la Makanisa na Mkutano wa Uislamu wa Kimataifa huko Colombo mji mkuu wa Sri Lanka.

Nawakaribisha kwa mara nyingine tena na ninakutakieni makazi mema nchini Misri, na ninawashukuruni kwa ukarimu wenu wa hii ziara ambayo imo ndani ya moyo wa kila Mmisri wa kiume na wa kike.

Ahsanteni kwa Kusikiliza.

Amani iwe kwenu na rehema za Mungu na Baraka zake.

     KIPANDE HAKIKUINGIZWA NDANI YA HUTUBA

Lakini mfumo wa Utaifa haraka ulibadilika baada ya kupanuka ufunguzi wa miji ya Kiislamu na kuboreka mahusiano ya Waislamu kwa wenzao wasio kuwa Waislamu ndani ya miji iliyofunguliwa, na ikawa lazima kuonesha uhusiano kwa asiyekuwa Mwislamu ndani ya dola la Kiislamu, na hapa ukazaliwa msamiati “watu wa mkataba” ambapo unamaanisha kuwa Mkristo na Myahudi wapo katika dhima ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake ambapo haki na wajibu zinakuwa sawa.

Print
5237 Rate this article:
No rating

Please login or register to post comments.

أقسم بالله العظيم أن أكون مخلصًا لديني ولمصر وللأزهر الشريف, وأن أراقب الله في أداء مهمتى بالمركز, مسخرًا علمي وخبرتى لنشر الدعوة الإسلامية, وأن أكون ملازمًا لوسطية الأزهر الشريف, ومحافظًا على قيمه وتقاليده, وأن أؤدي عملي بالأمانة والإخلاص, وأن ألتزم بما ورد في ميثاق العمل بالمركز, والله على ما أقول شهيد.