Afrikaans (Suid-Afrika)

منبرٌ كبيرٌ لنشر وسطية الأزهر الشريف بكل لغات العالم

 

Taarifa ya haraka baada ya Sala ya Ijumaa ...  Imamu Mkuu Sheikh Al-Azhar kwa watu wa Jerusalem:
Anonym
/ Categories: Main_Category

Taarifa ya haraka baada ya Sala ya Ijumaa ... Imamu Mkuu Sheikh Al-Azhar kwa watu wa Jerusalem:

Taarifa ya haraka baada ya Sala ya Ijumaa ...

Imamu Mkuu Sheikh Al-Azhar kwa watu wa Jerusalem:

Kuwe kupigania kwenu kwa kiwango cha imani yenu, kwa kadhia yenu na mapenzi yenu kwa nchi yenu… na sisi tupo pamoja nanyi na hatutawaacheni.

 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu.

Al-Azhar Al-Sharif inafuatilia kwa hasira kubwa, kukana na kupinga yale yaliyosemwa na Idara ya Marekani juu ya tangazo la Mji wa Jerusalem Mtakatifu kuwa ni mji mkuu wa jamii ya Wazayuni, ni hatua ya uporaji haujawahi tokea na ukiukaji mbaya wa makubaliano ya kimataifa na uibuaji hisia ya Waislamu zaidi ya bilioni moja na nusu duniani, na uibuaji pia wa hisia za mamilioni ya Waarabu Wakristo ambao ndani ya kipindi kirefu cha historia Misikiti mikongwe na Makanisa makongwe yamewakutanisha pamoja na ndugu zao Waislamu.

Sisi ndani ya Al-Azhar Al-Sharif, na kwa jina la ulimwengu wote wa Kiislamu tunasisitiza kupinga kwetu moja kwa moja hatua hii isiyofaa kisheria na kikanuni, kama vile tunasisitiza kuwa kupigwa hatua katika kuliendea jambo hili kunakuwa ni udanganyifu wa wazi wa historia usio kubalika, lakini pia ni uovu kwa mustakbali wa wananchi, hauwezi kunyamaziwa kabisa madamu mapigo ya moyo wa Waislamu bado yanapiga.

Watu wote wafahamu… hakika ya Jerusalem ni mji mkuu wa nchi ya Palestina inayokaliwa kwa nguvu na jamii ya kimabavu ya Wazayuni waporaji, na wala haitokuwa kinyume na hivyo, na harakati zozote zinazopingana na hali hiyo zinapingwa na mwisho wake utakuwa ni mbaya.

Hakika tunatahadharisha kwa nguvu zote hatari ya msimamo wa kushikilia uamuzi huu batili ambao unawasha moto wa chuki kwenye nyoyo za Waislamu wote na katika nyoyo za wapenda amani duniani, lakini pia ni tishio hatari la amani na usalama wa kimataifa.

Na wafahamu pia watu wa ngazi za maamuzi wa Kimarekani kuwa, siasa ya kipimo kimoja kwa vipimo viwili na kitendo cha usaidizi mkubwa wa mabavu ya Wazayuni makatili pamoja na kuondoa haki ya wananchi na urithi wa mataifa na ustaarabu wake, ni siasa si ya kistaarabu na wala hazitabakia wakati wowote ule, na kubakia kadhia ya Jerusalem ya Kiarabu ndiyo kadhia ya kwanza ya Waarabu na Waislamu ambayo haitakufa milele.

Sisi kutokea hapa nchi ya Misri ya Al-Azhar, Misri ya Kiarabu na Kiislamu … tunatoa wito kwa viongozi na serikali za ulimwengu wa Kiislamu, Umoja wa nchi za Kiarabu, Shirikisho la nchi za Kiislamu na Umoja wa Mataifa kuchukua hatua za haraka na za dhati kusimamisha utekelezaji wa hatua hii na kuitupia mbali.

Kama vile tunatoa wito kwa nguvu zote, kwa Jumuiya zote za Kimataifa zenye kupenda amani na kupambana na siasa za ukoloni kuchukua hatua za kusimamisha janga hili la Kimataifa na la kibinadamu ambalo linachukua nafasi katika ulimwengu wetu.

Kama vile tunatoa wito kwa wananchi wa Ulimwengu wa Kiarabu na Kiislamu kupinga mikakati hii miovu ya Wazayuni wa Kimarekani, na kurejesha mwamko wa Kiarabu na Kiislamu katika kadhia ya Jerusalem Takatifu ambayo ni Qibla ya kwanza na sehemu ya tatu takatifu na pia ni sehemu aliyopelekwa usiku mwisho wa Manabii na Mitume..

Na mwisho kabisa tunasema kwa watu wetu wa Jerusalem… tunauhuhisha msimamo wenu wa ujasiri, na kuufunga kwenye mikono yenu, na uwe utetezi wenu wa tatu kwa kiwango cha imani yenu kwa kadhia yenu na mapenzi yenu ya nchi yenu, na sisi tupo pamoja nanyi na wala hatutawaacha… na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kushinda juu ya jambo lake lakini watu wengi hawajui…

(Na ikifika ahadi ya mwisho ili waziharibu nyuso zenu, na waingie Msikitini kama walivyo ingia mara ya kwanza, na waharibu kila walicho kiteka kwa uharibifu mkubwa)…. Amesema kweli Mwenyezi Mungu Mtukufu.

 

Print
6283 Rate this article:
No rating

Please login or register to post comments.

أقسم بالله العظيم أن أكون مخلصًا لديني ولمصر وللأزهر الشريف, وأن أراقب الله في أداء مهمتى بالمركز, مسخرًا علمي وخبرتى لنشر الدعوة الإسلامية, وأن أكون ملازمًا لوسطية الأزهر الشريف, ومحافظًا على قيمه وتقاليده, وأن أؤدي عملي بالأمانة والإخلاص, وأن ألتزم بما ورد في ميثاق العمل بالمركز, والله على ما أقول شهيد.