1- Sheria zote za mbinguni zimeafikiana kuhusu maadili ya kibinadamu, na kwamba yeyote atakayevunja maadili hayo basi atakuwa hajakwenda mbali na muktadha ya dini tu, bali amekwenda mbali na ubinadamu wake na maumbile sawa alilowaumbia watu na Mwenyezi Mungu.
2- Dini ya Kiislamu inatufundisha kwamba tunapaswa kusema kauli njema kwa watu wote bila ya kuwatofautisha, Mwenyezi Mungu Mtukufu Amesema: {Na mseme na watu kwa wema}. Siyo hiyo tu, bali sisi tunatakiwa kusema maneno yaliyo mazuri zaidi, Mwenyezi Mungu Amesema: {Na waambie waja wangu waseme daima maneno yaliyo mazuri}.
3- Usamehevu ni wito mkuu katika sheria zote za mbinguni, ili wanadamu waishi katika amani na usafi wa moyo, pasipo na ugomvi, utengano, vurugu wala ugaidi.
Kituo cha Al-Azhar cha Kupambana na Mawazo Makali
Kitengo cha Lugha za Kiafrika