• Ugaidi ulioenea ulimwenguni ukiachwa kukua na kupata nguvu basi wanadamu wote watarudi kwa hali ya fujo na unyama.
• Vita vya kisasa havikusidii maadui wa nje, bali vianlengea wananchi wasio na hatia baada ya kuuandaa ulimwengu kwa maeneo ya migogoro ya kimadhehebu na kidini.
• Watakaonufaika kwa vita waliweza kutumia dini kama ni kuni ya kuchoma na kukuza vita na uharibifu.
• Kujiokoa kutoka mifumo ya kisaliti haiwezikani kuwa hoja ya kuwapiga wananchi wasio na hatia kwa ndege na kuzibomoa nyumba zao.
• Dini na madhehebu si kitu kipya bali zimepata kuishi na amani chini ya uongozi wa ustaarabu wa kiislamu bila ya kudharauliwa kiitikadi wa kimapato.
• Nimetafuta katika mabara yote duniani ili kufikia eneo linalozingatiwa kama ni mahali pa matumizi mengi ya silaha na umwagaji damu nikagundua kwamba maeneo ya kiarabu na kiislamu ni mahali pa kimsingi pa mateso haya.
• Bodi la Umoja wa Mataifa lililoanzishwa kwa ajili ya kulinda amani na usalama za kimataifa linaweza kuchangia kuyatatua matatizo ya mashariki ya kati na kumaliza mateso yake.
• Uislamu hasa - na dini zote - haiwezekani kabisa kuwa ni sababu ya maangamizi hayo yanayojiri na yasiyodhibitiwa.
• Tunapaswa kutafuta sababu za kutoweka amani katika mwelekeo wa staarabu kuu za kisasa ambazo hazioni dhiki katika kubuni adui asiyekuwepo kwa ajili ya kumtumia kama ni kisingizio cha kuzuka vita mbali na nchi zake.