Afrikaans (Suid-Afrika)

منبرٌ كبيرٌ لنشر وسطية الأزهر الشريف بكل لغات العالم

 

MAELEZO YA  JOPO KUU LA WANACHUONI AZHAR SHARIF
Anonym
/ Categories: Main_Category

MAELEZO YA JOPO KUU LA WANACHUONI AZHAR SHARIF

 

Jopo Kuu la Wanachuoni wa Azhar Sharif linatangaza kuwa hatua zote ambazo zimechukuliwa na serikali ya kimabavu ya Wazayuni katika eneo takatifu la Qudsi ni batili kisheria na kikanuni, na wala hatua hizo hazina mashiko katika msingi wowote wa kibinadamu au kiustaarabu, na kutokana na hilo Azhar Sharif na kwa jina la Waislamu bilioni moja na milioni mia saba duniani inapinga vitendo hivi vya uchokozi, na ambavyo vimepelekea utendaji wake na Wazayuni kukiuka makubaliano yote ya kimataifa.

Na kurudisha kumbukumbu kuwa eneo takatifu la Qudsi na Msikiti wa Aqsaa ambao umebarikiwa na Mwenyezi Mungu kama ilivyokuja katika Qurani Tukufu ni Qibla ya kwanza na msikiti wa tatu mtukufu ni sehemu aliyopelekwa usiku Mtume wa Uislamu na Waislamu S.A.W. na ni mmoja ya msikiti ambayo misafara hutembelea kwenye msikiti huo.

Kama vile Azhar inazitaka nchi kubwa duniani, shirikia la UNESCO, majopo ya Kiislamu na ya kimataifa pamoja na mashirika ya utetezi wa haki za binadamu kusimamia majukumu yao katika kukomboa majumba ya Mwenyezi Mungu katika eneo la Qudsi na Palestina na sehemu zengine za ibada ulimwenguni kutokana na kushikiliwa kisiasa na kibaguzi…

Na Azhar inautahadharisha ulimwengu wote kutokana na kukaa kimya na kunyamazia vitendo hivi vya uadui ambavyo vinafungua tena upya milango ya vita vya kidini, na kutishia amani ya dunia na kuharibu kijani na sehemu kavu.

Kwa sababu hiyo, Azhar Sharif inatoa wito kwa taasisi za kisayansi na kielimu pamoja na Wizara za Waqfu kwa nchi zote za Kiislamu kuongeza umuhimu na uzito wa kadhia ya Qudsi na Palestina katika mitaala ya masomo na malezi pamoja na hotuba za Ijumaa kwenye misikiti mbalimbali na kwenye programu za kitamaduni na habari.

Azhar inatambua na kuthamini kuungana kwa makanisa pamoja misikiti kwenye ardhi inayokaliwa kimabavu, na kuinua adhana toka makanisa hayo, pamoja na kulazimishwa kuwa kimya na kupigwa marufuku kutoa adhana kwenye minara ya kuadhinia ya misikiti, ni ushindi wa Wakristo wa maadili ya kiroho na msingi wa ujirani mwema pamoja na kuheshimiana kati ya Waumini wa dini za mbinguni.

Azhar Sharif imechukua uamuzi wa kuitisha mkutano wa kimataifa kuhusiana na Qudsi mwishoni mwa mwezi wa tisa unaokuja - Mungu akipenda - mkutano huo utaangalia maamuzi muhimu kuhusiana na kadhia ya Kipalestina, na itaanza na mawasiliano na taasisi na mashirika yenye uzito na mambo haya.

Azhar wala haisahau kuwakumbusha wote juu ya mwisho mbaya wa watu wenye kiburi, na hakika Mwenyezi Mungu vyovyote Atakavyowapa muda kwa hakika hatawaacha bila ya malipo, na kubakia Qudsi na msikiti wa Aqsaa ndani ya mioyo ya Waislamu na kuwa ni kadhia yao ya kwanza.   

Print
5763 Rate this article:
2.0

Please login or register to post comments.

أقسم بالله العظيم أن أكون مخلصًا لديني ولمصر وللأزهر الشريف, وأن أراقب الله في أداء مهمتى بالمركز, مسخرًا علمي وخبرتى لنشر الدعوة الإسلامية, وأن أكون ملازمًا لوسطية الأزهر الشريف, ومحافظًا على قيمه وتقاليده, وأن أؤدي عملي بالأمانة والإخلاص, وأن ألتزم بما ورد في ميثاق العمل بالمركز, والله على ما أقول شهيد.