Afrikaans (Suid-Afrika)

منبرٌ كبيرٌ لنشر وسطية الأزهر الشريف بكل لغات العالم

 

Taarifa ya Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu wa Al-Azhar Al-Sharif
Anonym
/ Categories: Main_Category

Taarifa ya Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu wa Al-Azhar Al-Sharif

Taarifa ya Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu wa Al-Azhar Al-Sharif

Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu wa Al-Azhar Al-Sharif wamefanya mkutano wa dharura leo hii siku ya Jumanne mwezi 23 Mfunguo sita (Rabiul Awal) 1439 A.H. ambayo ni sawa na tarehe 12 Disemba 2017 A.D. chini ya uongozi wa Mheshimiwa Imamu Mkuu Prof. Ahmad Al-Tayyib, Sheikh wa Al-Azhar Al-Sharif, kwa ajili ya kuzungumzia uamuzi wa Marekani wa kuutangaza mji wa Qudsi (Jerusalemu) kuwa ni mji mkuu wa dola vamizi la Kizayuni, na mkutano wake kumalizikia kwa mambo yafuatayo:

Kwanza: Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu wa Al-Azhar Al-Sharif inakataa katakata maamuzi ya utawala wa Marekani yenye kukirihisha, maamuzi ambayo hayana mapokezi ya kihistoria au ya kisheria. Na yaliyotangulia kutangazwa na Sheikh wa Al-Azhar Al-Sharif ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Busara la Waislamu yanasisitiza kukataa kwake dhidi ya maamuzi haya. Kikao cha makamo wa Rais wa Marekani Bw. Mike Banz, ambacho kimekuja katika muktadha wa misimamo ya Al-Azhar ya kihistoria kuhusu suala la Palestina, kikielezea hisia za zaidi ya Waislamu bilioni moja na milioni mia saba, kama pia Kamisheni hiyo inavyoushukuru uamuzi wa Kanisa la Kitaifa la Kikoptiki la Misri katika msimamo wake huo huo. Papa Tuwadrous amekataa kikao cha Makamo wa Rais wa Marekani baada ya maamuzi haya batili.

Pili: Kwa hakika Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu inatilia mkazo kwamba maamuzi kama haya ya kijeuri na yenye kuipotosha historia hayatoweza kubadilisha chochote katika uhalisia ulivyo. Kwa sababu mji wa Qudsi (Jerusalemu) ni mji wa Palestina ya Kiarabu na ya Kiislamu. Ukweli huu hautofutwa na maamuzi ya kifedhuli wala hautopotezwa na makubaliano ya upendeleo wa kidhalimu.

Tatu: Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu inatoa wito kwa serikali zote na mashirika yote ya Kiarabu na Kiislamu kutimiza wajibu wao kwa mji wa Qudsi (Jerusalemu) na Palestina na kuchukua hatua zote za lazima za kisiasa na kisheria kwa ajili ya kuyabatilisha maamuzi haya. Kamisheni hii pia inazitaka serikali zote na taasisi zote za kimataifa na Baraza la Usalama na Umoja wa Mataifa, na kila walio huru na wenye akili ulimwenguni kuchukua hatua za vitendo na za kikweli-kweli ili kuling’oa shauri lolote la kisheria la uamuzi huu wa dhuluma. Na katika suala hilo hilo, Kamisheni hiyo inaisifu misimamo ya mataifa yote yaliyohuru na serikali mbalimbali zinazohusika ulimwenguni ambazo zimekataa maamuzi ya Marekani, hasahasa msimamo unaoongozwa na Umoja wa Ulaya, Urusi na Uchina, kama pia zinavyounga mkono Intifada ya Palestina inayotekelezwa na Wapalestina kwa kutoa fidia damu zao kwa ajili ya maeneo yao matakatifu, na inatoa wito kwa wenye uwezo, Waarabu na Waislamu, kutoa misaada ya kifedha kwa ajili ya Wapalestina.

Nne: Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu inatoa wito kwa taasisi zote za kielimu na kimalezi pamoja na wizara za mambo ya waqfu na ofisi za Mufti katika nchi za Kiarabu na Kiislamu kutilia umuhimu suala la Qudsi (Jerusalemu) na Palestina katika mitaala ya masomo na malezi na hotuba za Ijumaa na programu za kitamaduni, kielimu na kihabari; ili kurejesha mwamko kuhusu suala hili muhimu na hatma yake. Na katika lengo hili, Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu imeamua kuunda tume kwa ajili ya kutengeneza mtaala maalumu kuhusu suala la Palestina, mtaala ambao utasomeshwa katika ngazi zote za elimu ya Al-Azhar, na utatangaziwa katika mkutano wa Al-Azhar na Baraza la Wazee wa Busara la Waislamu ambavyo ni vyombo vya kimataifa ili kuunusuru mji wa Qudsi (Jerusalemu).  

Tano: Kamisheni hii inasisitiza kwamba Uarabu wa Qudsi na utambulisho wake wa kipalestina haukubali mabadiliko au kuchafuliwa, na kwamba mikataba ya Umoja wa Mataifa inaulazimisha utawala poraji wa Kizayuni kutogusa mazingira hayo juu ya ardhi hiyo na kuzuia hatua zozote zinazokiuka mikataba hiyo. Na ni wajibu wa utawala wa Marekani kuwa na mwamko kwamba utawala huo sio wa kibeberu ambao utakuwa unaitawala dunia, na kuwaamulia mambo watu wa mataifa mbalimbali, haki zao na maeneo yao matakatifu.

Sita: Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu inaonya kutokana na majaribio ya kujenga mahusiano na utawala wa Kizayuni kabla ya kuondoka katika ardhi za Kiarabu zinazoshikiliwa kimabavu na kusimama kwa dola la Palestina lililo huru na mji mkuu wake kuwa ni Qudsi (Jerusalemu) tukufu.

Saba: Ofisi ya Kamisheni ya Wanachuoni Wakuu inaendelea kufanya vikao vya mara kwa mara ili kufuatilia kwa karibu mabadiliko yanayoendelea, pamoja na kuandaa mapendekezo ya lazima kwa ajili ya kuyawasilisha kwenye mkutano kimataifa kwa ajili ya kuunusuru mji wa Qudsi (Jerusalemu), mkutano ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 17 na 18 Januari ijayo kwa kushirikiana na Baraza la Wazee wa Busara la Waislamu.

Print
5518 Rate this article:
No rating

Please login or register to post comments.

أقسم بالله العظيم أن أكون مخلصًا لديني ولمصر وللأزهر الشريف, وأن أراقب الله في أداء مهمتى بالمركز, مسخرًا علمي وخبرتى لنشر الدعوة الإسلامية, وأن أكون ملازمًا لوسطية الأزهر الشريف, ومحافظًا على قيمه وتقاليده, وأن أؤدي عملي بالأمانة والإخلاص, وأن ألتزم بما ورد في ميثاق العمل بالمركز, والله على ما أقول شهيد.