Kuna baadhi ya maoni finyu ambayo hayakubaliki kamwe yanayoashiria kuwa ukafiri unaruhusia mapigano, na kwamba waislamu wanapaswa kuwapigania watu ili wawalazimishe kujiunga na Uislamu, au wabaki na dini yao pamoja na kulipa dhamana "Jizya", maoni hayo ni batili kwani hayaafikiani na aya za Qurani wala Sunnah za Mtume (S.A.W.) hata kidogo, je, kwa nini Uislamu umeharamisha kuwaua wanawake, watoto na wazee ingawa wao ni makafiri?!