Leo.. Imamu Mkuu akutana na Mkuu wa Bunge la kifaransa na Mkuu wa Jumuiya ya kinyeji nchini Ufaransa
Mheshimiwa Imamu mkuu profesa; Ahmad Al-Tayib, Sheikhi mkuu wa Al-Azhar Al-Shareif na mkuu wa Baraza la wakuu wa waislamu, akutana leo Alhamisi, na Mkuu wa Bunge la kifaransa Gerard Larcher, vile vile yule Mheshimiwa atakutana na Mkuu wa Jumuiya ya kinyeji ya kifaransa Claude Bartolone kwa ajili ya kujadili juhudi za kupambana na mawazo makali na ugaidi.
Vile vile, Mheshimiwa Imamu Mkuu atajadili katika mikutano hiyo miwili njia za ushirikiano baina ya Al-Azhar Al-Shareif kwa upande mmoja na Jumuiya ya kinyeji ya kifaransa na Bunge la kifaransa kwa upande mwingine, pamoja na kuzungumzia mbinu za kuwafanya wafaransa wasilamu waingiliane na jamii yao.