Imamu Mkuu wa Al-Azhar: Tuko tayari kutoa ufadhili wa masomo usio na kikomo kwa wanafunzi wa Afrika Kusini ili kusoma huko Al-Azhar.
Tunathamini nafasi ya Afrika Kusini na msimamo wake wa kihistoria katika kuunga mkono suala la Palestina
Mheshimiwa Imamu Mkuu alisema: Msimamo wa kihistoria wa Afrika Kusini kuelekea uvamizi wa Wazayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza unaweza tu kutolewa kutoka watu wakubwa waliolelewa na kiongozi mkuu na shujaa, akiongeza: "Nina furaha kwamba sauti hii ya kipekee inatoka Afrika, hasa kutoka Afrika Kusini, ambayo ilisimama dhidi ya dhuluma na ukoloni na iliushinda, tuliishi enzi za Nelson Mandela, na tulipitia changamoto alizokabiliana nazo, na tukamchukulia kama ishara ya uthabiti, na alikuwa shujaa katika misimamo yake yote, kwani aliishi maisha yaliyojaa ushujaa, alikuwa shujaa alipoukataa ukoloni, alikuwa shujaa alipokataa ubaguzi wa rangi, alikuwa shujaa alipohimili kifungo kwa muda mrefu, na alikuwa shujaa zaidi alipowapandikiza watu wa Afrika Kusini maadili ya kuwaunga mkono wanyonge na kusimama mbele ya dhulma na madhalimu.
Sheikh wa Al-Azhar amethibitisha leo Jumapili wakati wa mkutano wake na Mheshimiwa Joseph Mashambai, Balozi wa Jamhuri ya Afrika Kusini mjini Cairo, kwamba kile ambacho Afrika Kusini imefanya ni silaha chungu zaidi kwa mamlaka ya Kizayuni, na ni msukumo wa harakati hii ya kimataifa iliyofanyika katika mitaa ya Ulaya na Amerika na vyuo vikuu vyake, akiashiria kwamba hatua ya Afrika Kusini kuelekea uvamizi dhidi ya Ghaza iliufanya mamlaka ya Kizayuni kupoteza sehemu kubwa ya hila zake ambazo inazichukua kama ulinzi kwa hoja ya chuki dhidi ya Uyahudi, na kuwahadaa watu wengi kwa miongo kadhaa. Lakini Afrika Kusini ilifichua uwongo huu na kuonyesha taswira ya kweli na mbaya ya mamlaka hii ya Kizayuni.
Sheikh wa Al-Azhar alituma ujumbe kwa watu wa Afrika Kusini: "Nyinyi ndio mlioamsha dhamiri ya ulimwengu ulio huru, mkarekebisha njia mbaya ambayo ulimwengu ulikuwa unaifuata, na mkawa pamoja na Wapalestina ishara ya uhuru, usawa, na makabiliano ya mashambulizi dhidi ya nchi, ardhi, na binadamu, sisi katika Al-Azhar tunathamini msimamo weno wa kihistoria katika kuunga mkono suala la Palestina, na tunajua kwamba mtakabiliwa na manyanyaso makubwa na changamoto, na mtalipa gharama kubwa, na sisi tuko tayari kutoa ufadhili wa masomo bila kikomo kwa Waafrika Kusini ili kusoma katika Al-Azhar, kwa kuthamini nafasi hii ya kipekee ya kihistoria.
Kwa upande wake, balozi wa Afrika Kusini alionyesha furaha yake katika kukutana na Sheikh wa Al-Azhar, na shukrani ya nchi yake kwa uungaji mkono wa Al-Azhar kwa msimamo wa Afrika Kusini mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu, akitangaza: "Tunafahamu kwamba kufikia amani haitakuwa rahisi, na nchi yetu iko tayari kusonga mbele katika njia hii kwa gharama yoyote", akibainisha kwamba Afrika Kusini inadumisha uhusiano imara na Al-Azhar, na kwamba jumuiya ya Waislamu nchini Afrika Kusini ina nafasi kubwa katika ukuaji na maendeleo katika nyanja mbalimbali.