Uzayuni...na Mradi wa Kuanzisha Nchi ya Kiyahudi

Imaendaliwa na Bw., Eslam Ragab Mohammed

  • | Thursday, 14 November, 2024
Uzayuni...na Mradi wa Kuanzisha Nchi ya Kiyahudi

Uzayuni ni kundi la kisiasa lililoibuka mwishoni mwa karne ya kumi na tisa BK ndani ya jumuiya za Wayahudi katika Ulaya, na lilitokana na wazo la kuunda nchi ambayo itamaliza hali ya kutangatanga ambayo Wayahudi walikuwa wameishi tangu ya ufalme wa Ashuria, kwa mujibu ya Talmud, na inawauruhusu watu wa Kiyahudi kurudi kwa nchi ya asili au nchi ya ahadi (Palestina).

Misingi ya kisiasa

Kundi la Kizayuni lilianzishwa juu ya fikra ya kuwakusanya Wayahudi wote ulimwenguni na kuanzisha taasisi au vyombo vya kisiasa ambavyo vitawahakikishia jambo la kupambanua Wayahudi na kubadilisha mtazamo wa kijamii kwa Wayahudi na kuwalinda dhidi ya hatari ya kuchanganya ndani ya jamii za Ulaya ambamzo waliishi ndani yake kama  ni watu wachache wanaotengwa, wanaodharauliwa na hubaki mbali na maisha ya kisiasa na kiuchumi.

Uzayuni unaamini kwamba marejeo yaliyoahidiwa hayatapatikana isipokuwa kwa juhudi za Kiyahudi tu ambazo hazina msaada wowote isipokuwa msaada wa Mwenyezi Mungu, kwani maana ya Uzayuni ni ufufuo wa kisiasa wa Wayahudi kupitia kurudi kwao wote kwa Palestina, au kwa maneno mengine ni kutoa umbo wa kisiasa na kitaifa kwa Uyahudi.

Herzl ndiye aliyeanzisha kundi la Wazayuni na mmiliki wa mradi wa nchi ya Kiyahudi, ambayo aliiuzungumzia kwa kirefu katika kitabu aliyekiandika mwaka 1896, kwa unuani “Nchi ya Kiyahudi” ambamo aliwasilisha mawazo yenye ufanisi ambayo yataweza kuchanganya katika mafanikio ya mradi baadaye, Mawazo haya yalihusu kuwahamisha Wayahudi kwenda Palestina, kuhamasishwa kwa sababu ya suala la Kiyahudi kote ulimwenguni, na kisha kuwajaalia Wayahudi wanakwenda nyuma ya wazo la nchi ya Kiyahudi, ambayo haikuwa muhimu kwa vikundi vikubwa vya Wayahudi.

Hatua ya kwanza muhimu katika mradi wa Kizayuni ilihusishwa na chama kilichoanzishwa na wanafunzi wa Kiyahudi katika mji wa Kharkiv wa Kiukreni mnamo 1882 na kukiita Jumuiya ya "Belo" Chama kilijiwekea lengo la vitendo ambalo lilikuwa rahisi kutekeleza na la juu sana katika kufanikisha mradi wa Wazayuni, ambalo lilikuwa ni kuanzisha mikusanyiko ya kilimo kwa Wayahudi wa Mashariki huko Palestina.

Mkutano wa Basel

Harakati ya Kizayuni ilipata mvuto mkubwa wa kisiasa na vyombo vya habari barani Ulaya na duniani kote kwa mkutano wake wa kwanza uliofanyika kati ya tarehe 29 na 31 Agosti 1897 katika mji wa Basel wa Uswizi.

Mkutano huo ulihitimishwa na kazi yake ya kutangaza kuanzishwa kwa kundi la Kizayuni Ulimwenguni na kuichagua kamati ya utendaji yenye makao makuu mjini Vienna. Taasisi hizi ziliimarishwa na mkono wa kifedha ambao ni Mfuko wa Kiyahudi, ambao ulianzishwa kwa kuzingatia maamuzi ya Mkutano wa Tano mnamo 1901.

Sambamba na hatua hii, mawimbi ya uhamiaji wa Wayahudi wa Mashariki kwenda Palestina yaliendelea, hasa kutoka Urusi baada ya Mapinduzi ya Bolshevik yaliyoshindwa mnamo 1905.

Katika kutafuta uungwaji mkono miongoni mwa mataifa makubwa ya wakati huo, Herzl alikwenda nchi ya Kiothomani na alifanya mazungumzo nayo (kati ya 1896-1906) ili kutoa hati ya kuwapa Wayahudi haki ya kurejea Palestina, na alionyesha kujiingilia kati kwenye mamlaka ya Ulaya ili kupunguza deni kubwa la nchi ya Kiothomani.

Lakini mazungumzo hayakufikia matokeo, kwa hivyo Herzl aliamua kwenda Uingereza na aliweza kupata fursa ya kuwasilisha tatizo la uhamiaji (pamoja na uhamiaji wa Wayahudi) mbele ya "Baraza la Commons", alianzisha mawasiliano ya karibu na wanasiasa wa Uingereza akiwemo waziri Joseph Chamberlain, ambaye alipendekeza kuanzisha mkusanyiko wa Wayahudi huko Al-Arish au Uganda. Ingawa ya kushindwa kwa juhudi hizi, basi zimeweza kuunda ushindi muhimu wa kisiasa, kwani zilijumuisha utambuzi wa Uingereza kwamba Wayahudi ni taifa lenye haki ya kujitawala juu ya eneo lao wenyewe.

Hatua za Herzl hazikubaliwa na Mzayuni wa Urusi Chaim Weizman (Rais wa Israeli kati ya 1949-1952), ambaye aliona kile alichokiita Uzayuni wa kidiplomasia kuwa ni hauna maana, na badala yake akapendelea kile alichokiita njia ya kifalme.

 Kwa hiyo, Weizmann alianzisha mawasiliano makubwa na mazingira ya karibu ya Mfalme wa Uingereza, na jitihada zake zilizaa matunda ya “Azimio la Balfour” la 2 Novemba, 1917, ambalo lilifungua njia kwa ajili ya kuanzishwa kwa Israeli baada ya miaka mitatu.

Sambamba na mafanikio hayo ya kisiasa mfululizo, taasisi za Kizayuni zilikuwa zinapanga uhamiaji kwenda Palestina ili wawe na idadi kubwa dhidi ya Wapalestina, lakini kundi la Kizayuni lilikabiliwa na changamoto nyingine, ambayo ilikuwa kukataliwa ndani ya jamii ya Kiyahudi yenyewe, kwani jamii ya Kiyahudi haikusadikishwa na wazo la nchi, na hakuna mabadiliko makubwa yaliyotokea katika Mwenendo huu isipokuwa baada ya kuangamizwa kwa Wayahudi mikononi mwa Wanazi katika Holocaust ya Vita vya Kidunia vya pili.

Ahadi kisha serikali

Nchi za kikoloni (hasa Uingereza na Ufaransa) yalibariki kuanzishwa kwa makazi ya Wayahudi huko Palestina, lakini Uingereza, mlezi wa Palestina, ilitaka kutoanzisha nchi ya Kiyahudi juu ya kunyima haki ya Wapalestina kuanzisha nchi yao.

Kuanzishwa kwa Israeli kuliwakilisha ushindi kwa wazo la nchi ya Kiyahudi, kama ilivyosemwa na Herzl, lakini kundi la Kizayuni lilianza kuchukua mwelekeo wa fikra kali ya ubaguzi wa rangi ambayo ilikua kwa miaka mingi, kwa sababu ya hitaji la kuwakusanya Mayahudi huko Palestina ili kuanzisha nchi juu ya magofu ya nchi ya Palestina na kisha kuwafukuza Waarabu na kuanzisha nchi ya Kiyahudi tu.

Kundi la Kizayuni, pamoja na Israel, imeainishwa kutoka sehemu nyingi za dunia kuwa ni Kundi na nchi ya kibaguzi, si kwa sababu ya misimamo yake juu ya Waarabu, bali kutofautisha kati ya Wayahudi wenyewe, na mifano ya hili ni kutengwa kwa Wayahudi wa Kihabeshi wa Falasha na Wayahudi wa Mashariki na Magharibi ya Kiislamu.

Print
Categories: Makala
Tags:
Rate this article:
1.0

Please login or register to post comments.